Tuesday, 10 December 2024

JE Unafahamu Laana ya Kutembea na Mume wa Mtu na Madhara Yake ?

 


Kutembea na mume wa mtu sio jambo zuri japo wanawake wengi wanaona ni kawaida bila kujua wanajilimbikizia laana itakayofanya maisha yao kuwa magumu mbeleni.

Machozi ya uchungu ya mwanamke mwenzio juu ya mume wake hayafutiki haraka.. Ni kama zigo la kinyesi mgongoni linavutiwa na inzi pekeake.

Huyo mwanaume unaemuona Leo ana mke, Pesa na mali na kuona ndo fursa kwako kumpata kwasababu anajua kujali na anapesa za kutosha kukugharamia.... Ukirudi nyuma miaka 10-15-20 mwanaume huyo huyo alikuwa kama huyu unae mkataa leo

Unaye muona hajui kuvaa.... Hana pesa za kutosha.. Hana mali kwahiyo hakufai.

Wanaume wengi wanaanzia chini... Jitihada za wake zao zinawafikisha walipo Leo. Heshimu jitihada hizo.

Heshimu siku walizofunga kwa ajili ya waume zao.
Heshimu machozi waliomlilia Mungu awafikishe walipo...
Heshimu muda na jasho walilolitoa kuhakikisha waume zao wanaonekana watu mbele za watu.

Muombe Mungu akupe wa kwako hata kama masikini mpate utajiri pamoja. Na wewe ubige magoti , ulie na kufunga.

Wanawake wengi wanalalamika hawaolewi au Wachumba wanawaacha bila sababu za msingi. Wanasahau zigo la kinyesi walilobeba mgongoni. Mwanamke piga magoti muombe Mungu akusamehe kwa kumliza mwanamke mwenzio.

Tuwaombee watoto wetu na kuwaonyesha njia iliyo bora. Kuwafundisha dini ili wawe na mahusiano mazuri na Mungu... wasikumbwe na laana hii.

Ewe mama elimisha watoto wako. Ewe dada elimisha wadogo zako.

Tukishirikiana kwa pamoja tutayafuta machozi ya wanawake .

TUPE MAONI YAKO HAPA

Tuesday, 17 September 2024

KISA Cha Kusikitisha 'Baba Yangu Alisababisha Nilale na Mjomba Wangu, Kamwe Sitamsamehe'

 KISA Cha Kusikitisha 'Baba Yangu Alisababisha Nilale na Mjomba Wangu, Kamwe Sitamsamehe'

Nimeona leo nitoe siri yangu hapa ya muda mrefu ambayo imekuwa ikiniumiza sana pale tu ninapokumbuka, nakosa raha na amani inapotea.

Kwa ufupi kabisa, nilizaliwa mkoani Mara wilaya ya Musoma mjini maeneo ya Nyakato, mama yangu alibeba mimba yangu akiwa darasa sita hivyo hakumaliza shule. Ilibidi akae nyumbani mpaka pale alipojifungua, kwa wakati kulikuwa hakuna sheria kali kwa wanaowapatia wanafunzi mimba wakiwa shule. Na aliyempatia hiyo mimba naye alikuwa mwanafunzi mwenzake lkn alikuwa la saba yeye alimaliza shule. Baba yake mama ambaye ni babu yangu alikuwa na uwezo mkubwa hivyo hakushindwa kutulea mimi na mama.

Nikiwa na miaka 6 ndipo nilipokuja kumjua baba yangu wakati huo nae alikuwa amekuwa mtu mzima, alikuja akanisalimia akaondoka, kwao pia walikuwa vizuri kimaisha.

Nikiwa na miaka 9 naanza darasa la kwanza wakati huo tulikuwa tunaingia shule tukiwa na umri mkubwa tofauti na sasa. Mama aliolewa na mume mwingine na alikuwa ni askari jeshi, alifanikiwa kuzaa nae watoto wanne jumla kwenye familia yetu tukawa 5 wasichana tukiwa wawili na wavulana wakiwa 3. Tuliishi vizuri sana, na familia ilikuwa na furaha sana na hatimaye tulijenga nyumba nzuri sana mtaa wa Majita road hapo hapo musoma. Nakumbuka nikiwa darasa la sita babu yangu kizaa mama alifariki duniani na ndiye aliyekuwa tegemeo la familia ya kina mama. Pia wakati huohuo baba yangu wa kufikia walikorofishana na mama kupelekea mpaka wakaachana na alihamishwa kuja Dar es salaam Lugalo. Sisi tulibaki Musoma tukiendelea na maisha.

Kumbuka wakati wote huo baba yangu mzazi ajaonekana kwa kipindi kirefu. Kwa upande wangu si kuwa na shida na nilifika mahali nikamsahu kabisa. Mama alikuwa anajituma sana alikuwa ana hotel yake hapo hapo Musoma hivyo alivyoachana na baba yangu wa kufikia akutetereka kiuchumi. Nilisoma na Mungu alinijalia kichwani nilikuwa vizuri toka darasa la kwanza nilikuwa nashika nafasi ya kwanza nikishuka sana nafasi ya pili mpaka la saba. Baada ya kuhitimu la saba Mungu alinijalia nikafahulu vizuri na kuingia kidato cha kwanza.


Wakati nikiwa kidato cha pili baba alikuja kutoka Arusha maana alikuwa anakaa huko, alipokuja alinikuta naendelea na masomo yangu vizuri. Alifika mpaka nyumbani nakumbuka mama alipomuona alimfukuza, wakaja watu kusuluisha na wazee kwamba ampe nafasi ya kumuona mwanae mama alikataa. Akamwambia wakati huo alikuwa wapi? Basi siku moja niko shule maana nilipangiwa hapo hapo Musoma sekondari, alifahamu ninapo soma kaja kaulizia walimu akanipata, niliitwa darasani nilipotoka nikamuona lakini sikumjua vizuri maana ni siku nyigi sana. Akanambia ni baba yako kwani umenisahau? Nilikataa kuongea lakini alinisihi sana mwisho nilikubali kuongea nae wakati anaondoka akanipa laki moja za matumizi akaondoka. Nilipofika nyumbani nilimpa mama hiyo pesa alishangaa nimetoa wapi, nikamwelezea yote basi mama akapokea. Kesho baba akaja akaomba msamaha hapo mama akamwambia kikubwa nataka umsaidie mwanao basi. Basi baba akaondoka.

Nilipofika kidato cha tatu mama alianza kuugua sana, tukaanza kuzunguka mahospitali kila akipimwa hakuna ugonjwa, tukaenda Bugando ugonjwa haukuonekana, tukaenda Muhimbili pia ugonjwa akuonekana kumbuka mama ndiye tegemeo la familia pesa za matibabu zilitoka kwake mpaka ikafikia hatua tukafilisika hotel ikafungwa hali ikawa mbaya sana. Tukaanza kuishi kwa shida sana. Tukashauriwa twende kwa waganga tukazunguka, alikuwa anapata nafuu kidogo kisha ugonjwa unarudi tena. Nikaanza kumtafuta baba ili atusaidie kila nikiongea nae kwa njia simu anatoa ahadi tu mwisho nikakata tamaa. Kwa baba wa kufikia aliyoko Dar nae alikuwa kimya sana alisahau hata familia yake kabisa. Hivyo tulikata tamaa kabisa na mababa hawa. Tukaamua kuishi maisha yetu bila kutegemea wao tena.

Nilisoma kidato cha nne kwa shida sana, tukitoka shule mimi na wandogo zangu tunaenda kutafuta vibarua vya kufanya ili tupate kula. Mpaka nikamaliza form 4, baada ya matokeo kutoka nikawa nimefahuru vizuri nikapagiwa shule ya advance huko Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro. Hapo ndipo ilikuja kesi ni wapi pa kupata pesa ya shule. Jamani umasikini mbaya sana, kama ujapitia mshukuru Mungu sana. Mama yangu wakati huo hali yake iliendelea kuimarika baada kwenda kwenye Maombi. Tuliangaika sana na mama lakini hatkufanikiwa kupata pesa ya kutosha.

Namshukuru Mungu kwa kipindi chote hicho sikuwahi kukutana na mume japo nilikuwa mzuri mtaani kwangu, walinisumbua mpaka waume za watu lakini hawakunipata. Lkn nilipata wazo nikasema baba yangu yuko Arusha na mm nimechaguliwa Mkoa wa Kilimanjaro ni mikoa iliyokaribu. Nilimpigia simu nikaongea nae nikamwambia nimefahalu lkn sina pesa akasema wakati unakuja shule pitia hapa Arusha nitakupa pesa za shule. Basi nikaona unafuu mkubwa, nikajianda maana muda ulikuwa ushafika. Arusha huko alikuwepo mjomba wangu tumbo moja na mama alikuwa askari wa FFU hapo Arusha lakini alikuwa na roho mbaya sana hawezi kumpa mtu msaada kirahisi. Nilimtaarifu pia kwamba nitakuja na nitafikia kwake alikubali.

Siku ya safari nilimtaarifu baba akasema sawa, nikamwambia nitafikia kwa Mjomba alafu ndio nakuja kwako kuchukua pesa za shule, tukakubaliana. Nilipofika Arusha majira ya saa 2 usiku mjomba alikuja akanipokea akanipeka kwake, mjomba alikuwa na mke na watoto wa 3, ila wakati nafika nilikuta mke wake ameenda kwao likizo, yupo mfanyakazi wa ndani na watoto, cha ajabu nilianza kutafuta baba kwenye simu akupatikana tena.

Nilikaa kwa mjomba siku 4 bila baba kupatikana kwenye simu sikuwa na pesa yoyote. Ikabidi nimwombe mjomba anisaidie angalau kidogo niende shule baba akipatikana akinipa nimrudishie mjomba alikataa katakata. Niliwaza sana sikujua ninzie wapi nilikata tamaa ya kusoma tena, ikabidi nimwombe mjomba nauli ya kurudia kwetu Musoma napo aligoma akasema subiri mpaka baba yako apatikane. Siku moja jioni katoka kazini akaniita chumbani kwake nilishutuka lakini akasema njoo nikupe pesa za shule, kweli nilipoingia ndani akanipa laki tatu, nikamshukuru sana sikuamini, nilipotaka kuondoka akanishika mkono akanitazama akanimbia naomba nilale na wewe usiku wa leo, niliogopa na kushituka sana, alifunga mlango akanitishia mwisho nilipoa akafanya anachotaka kufanya, aliniumiza sana maana sikuwahi kufanya kideto hicho. Baada ya kumaliza akanipa hizo pesa nikajianda kwenda shule kabla sijaenda akanifanya tena alinigeuza mke wake, sikumwambia mama yangu chochote maana angesikia yawezekana angekufa kabisa. Lakini yote hayo kwa sababu ya shida.

Nikafanikiwa kwenda shule, nilisoma vizuri na mjomba akawa anakuja hapo shuleni kuniletea pesa za matumizi siku za Jumapili nakunichukua kwenda gesti, maisha yangu yalikuwa hayo mpaka namaliza kidato cha sita, nikarudi nyumbani Musoma mama alifurahi sana aliposikia mjomba alinisomesha, lakini nilikuwa siri yangu. Mjomba alitaka nilirudi tena Arusha huku nikisubiri kwenda chuo kikuu. Nilikataa kabisa na mimi nilikuwa tayari nimetimiza malengo ya kishule sikuwa na hamu tena bali niliendelea kujutia dhambi niliyofanya.

Mungu alisadia nikapangiwa chuo cha Dar es salaam, nilipata mkopo hivyo ulinisaidia mpaka namaliza chuo, nikakutana na rafiki wa kiume mwanachuo mwenzangu, tulipohitimu tulifunga ndoa na sasa tuna watoto 2. Hii ni siri kubwa sijahawahi mwambia mume wangu. Baba aliposikia nimemaliza chuo akajitokeza, nilifukuza kwangu na kamwe sitaweza kumsamehe katika maisha yangu.
TUPE MAONI YAKO HAPA

Muda Mwingine Wanaume Kuchapiwa Wake zetu Tunatakaga Wenyewe

Hili suala nimelifikiria kwa kipindi kirefu sana., naona mifano mingi kupitia kwa marafiki zangu na hata ndugu zangu na watu wangu wa karibu. Unakuta mwanaume upo kwenye mahusiano ya kawaida na msichana bado hamjafunga ndoa alafu migogoro na kuachana mara kwa mara, tena unakuta wewe ndo unaachwa na huyo mwanamke alafu unambembeleza mnarudiana. Mwanamke haonyeshi upendo wowote kwako lakini wewe unaendelea kumpenda na kumjali sana. Hayo yote haujifunzi unaamua kumng'ang'ania na mwisho wa siku mnafunga ndoa.


Hivi mwanamke kama huyo akiwa anakusaliti katika ndoa utamlaumu nani.?
Kuna rafiki yangu wa karibu aliwahi kuoa mwanamke wa aina hiyo, ndoa yao ilidumu kwa miaka 5 tu na mimi nilikuwa best man wake, maana mwisho wa siku ikaja kugundulika hata watoto wawili ambao walikuwa wameshazaa hawakuwa wa kwake.


Wanaume tujifunze jamani tunapochagua mwanamke wa kuishi naye kwa maisha yote, tusiziendekeze akili za nyege wakati wa kuchagua wenzi wa maisha.
TUPE MAONI YAKO HAPA

Wakina Dada Mnaohudumia Saloon za Kiume Punguzeni Kidogo...Wengine Tuna Wake Nyumbani

 Wakina Dada Mnaohudumia Saloon za Kiume Punguzeni Kidogo...Wengine Tuna Wake Nyumbani

Hakika nawaambieni sisi wanaume kwa hizi Barbershop kuzikimbia inataka kama kuwa ngumu hivi?

Kwanza hawa kina dada wa Saloon za kiume wameteka sana soko then wanapenda sana Tip. Yaani imekuwa kama lazima kumbe ni hiari ya mtolewa huduma.

Halafu hawa Dada wajanja sana akitaka kukuhudumia mfano scrub anakufungua vishkizo vya juu then anapitisha mikono yake kifuani huku anakuburuzia na kucha zake ndefu kwa Nippon zako aise seriously lazima unyegeke tuu, then anamalizia kwenye masikio then anakuulizia vipi Una- Enjoy?

Huwa wanamikono lainiiiiiii hatari sana akikushika lazima utoe pesa tuu hata 30,000/= walahi. Kuna Barbershop hapo Sinza nilienda nikanyoa fresh baada ya kumaliza kuna huyo Sister akaniuliza unahitaji scrub? Nikakubali akasema twende ndani nimekaa tu kwenye kiti anarembua hatari, kanisugua masikioni, shingoni, akaniambia nitoe shati litachafuka daah nikatoa basi kanisuguaa hadi kifuani huku mmmmh nikaanza kama kusahau shida, baada ya hapo ananiuliza do u need extra service plz ni nzuri nitakuonesha aisee nilimpa pesa nikakurupuka ndukiii kubwa.

Nawaonea huruma wanawake waliiolewa wanaibiwa sana duuuh jifunzeni kuwafanyia scrub waume zenu nyumbani mnaibiwaa sana huku..
TUPE MAONI YAKO HAPA

Wednesday, 5 June 2024

Diarra Ataja Sababu ya KULIA ushindi Dhidi ya Azam

 Diarra Ataja Sababu ya KULIA ushindi Dhidi ya Azam


Kipa namba moja wa Yanga, Djgui Diarra ameitaja fainali ya Kombe la FA kuwa ni moja ya mchezo wake bora ndani ya misimu yake mitatu aliyoitumikia timu hiyo huku akimtaja Mohamed Mustafa kuwa kikwazo.


Yanga imetwaa taji lake la tatu la FA msimu huu dhidi ya Azam FC kwa penati (5-6) mchezo uliochezwa Uwanja wa New Amaan Complex Kisiwani Zanzibar.


Akizungumza na Mwanaspoti, Diarra alisema dakika 120 walizocheza uwanjani zilikuwa ni mara mbili kutokana na ugumu aliokuwa nao langoni licha ya kutokuwa na mashambulizi mengi lakini alikuwa anatumia akili kubwa kuwaelewesha mastaa wenzake ili wamalize kazi.


“Nimecheza fainali tatu za FA msimu wa kwanza dhidi ya Coastal Union tulicheza dakika 120 na kuibuka na ushindi kwa mikwaju ya penalti 4-1, wa pili dhidi ya Azam FC mechi ilichezwa Tanga na Keneddy Musonda aliimaliza mapema kabisa dakika ya 16,” alisema na kuongeza;


“Msimu huu umekuwa bora na mgumu kuwahi kutokea dakika 120 bora na za kupambana kwa pande zote mbili umahiri na ubora wa kipa wa Azam FC Mohammed Mustafa ulinipa mtihani mgumu kuwaelewesha wenzangu ni namna gani wanatakiwa wafanye ili kumfunga.” Alisema.


Diarra amesema alimsoma kipa huyo na kubaini kuwa alikuwa anacheza na saikolojia za mastaa wake hivyo alifanya kazi kubwa kuhakikisha anazungumza na wachezaji wenzake ili kutumia akili wakati wa kupiga penalti.


“Haikuwa rahisi kukosa penalti mbili za mwanzo kwa wachezaji wenzangu niliamni wengi wametoka mchezoni na kuamini mechi imekwisha hivyo nikawa na kazi ya ziada kuzungumza na wenzangu kwa vitendo nafurai mambo yakabadilika na sasa sisi ndio mabingwa mara tatu mfululizo,” alisema na kuongeza;


“Nilikuwa na furaha sana juzi furaha yangu ilinifanya niishi maisha ya Yanga ndani yangu ni timu ambayo imenijengea upendo mkubwa kuanzia wachezaji na mashabiki zangu nilipopata hisia hizo ndio chanzo cha mimi kulia kwa furaha.” Alisema Diarra.


SIRI YA UBORA


Akizungumzia ubora wake ndani ya misimu mitatu huku akishindwa kumpiku Ley Matampi wa Coastal Union, Diarra alisema msimu huu ulikuwa bora na wa ushindani kutokana na idadi ya makipa wa kigeni kuongezeka.


“Hakuna nilichopoteza kwani nimefanya kama nilivyofanya misimu miwili nyuma nimeiosaidia timu yangu kutetea taji kuzidiwa cleen Sheet na Matampi ni sehemu ya changamoto ya ubora wa wapinzani lakini kazi yangu nimeifanya kama inavyotakiwa,” alisema na kuongeza;


“Matampi na makipa wengine wageni msimu huu walikuwa bora wamenipa changamoto sina budi kusifia kile walichokifanya kila mmoja kwa wakati wake ameipambania timu yake na kila mtu kavuna alichokipanda tukutane msimu ujao.” Alisema Diarra.


Kipa huyo ambaye alitwaa tuzo ya kipa bora wa mwaka misimu miwili mfululizo tangu ametua Yanga.

TUPE MAONI YAKO HAPA

Wanawake/Wasichana wa Aina Hii ni Hatari Sana Kuwa Nao Kimapenzi

  


Demu wako wa zamani

Ni vizuri kutorudia mahusiano ya zamani na zaidi kama kwenye mahusiano yenu ya mwanzo mambo hayakuishia kwa uzuri. Sababu kuu ya msingi, kiukweli ni kwamba hakika mwanzoni mlikuwa hamuendani na ndio sababu ya iliyopelekea kuvunjika kwa mahusiano yenu, ndani ya hizo sababu kuna vitu vilivyopolekea kutokea kwa hayo, ukichunguza na kuziangalia kwa makini utagundua ni za asili na ambazo si rahisi kwa mmoja wenu kuzibadilisha sababu ni vitu au mambo ambayo yatakuwa ni ya damuni.

Dada wa rafiki yako kipenzi

Epukana na kujiingiza kwenye mahusiano na dada wa rafiki yako. Si tu kwamba utaweza kujiingiza kwenye uhasama na chuki kama mambo hayatakwenda sawa, ila pia utaweza kujiweka kwenye mazingira ya kujikuta siku moja unapigwa hata ngumi za uso sababu tu ulimuumiza dada yake. Pia, utaweza kumkosa mtu ambaye ndie alikuwa ni kimbilio lako kwa mambo mbalimbali pale ambapo itatokea wewe na dada yake mambo kutokwenda sawa, sababu hapo patakuwa na mgongano wa kimaslahi kwa huyo rafiki yako.

Wanawake wenye mambo mengi

Kiukweli, kutoka na watu kama hawa kinaweza kuwa ni kitu cha kufurahisha, ila mwisho wa siku itakuingiza kwenye matatizo. Mara zote kumbuka ni vyema kuwa salama kuliko kujuta. Usijiingize kwenye majaribu ambayo utakuja kuyajutia kwa maisha yako yote.

Wanawake wanaopenda hela kupitiliza (Wachunaji)

Kuwa mbali nao, labda kama unataka salio lako limalizike pasipo wewe kujifahamu. Naamini hili kila mmoja analifahamu na halihitaji darasa zaidi.

Demu wa zamani wa rafiki yako

Kama unathamini urafiki wako na mshikaji wako achana na habari ya kutoka na aliyekuwa demu wake. Mambo yanaweza kubadilika na kuwa kama au zaidi ya yaliyotokea kwa rafiki yako na ikaja kula kwako zaidi. Wakati mwengine inaweza tengeneza chuki kati yako na rafiki yako, huku akiamini kwamba ulikuwa unatoka au kumnyemelea demu wake toka zamani.

TUPE MAONI YAKO HAPA

Saturday, 1 June 2024

Mwanafunzi afariki kwa kunywa Kemikali Maabara ya Shule

 Mwanafunzi afariki kwa kunywa Kemikali Maabara ya Shule



Mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari St. Mary’s iliyopo Manispaa ya Mpanda, Luis Emmanuel (17), amefariki dunia baada ya  kunywa kemikali inayodhaniwa kuwa ni ethanol katika maabara ya shule hiyo akiwa na wanafunzi wengine wawili.

Katika tukio hilo, Luis alikuwa na Wanafunzi wenzake wawili wa kidato cha nne katika shule hiyo wakifanya usafi katika maabara ya kujifunzia masomo ya sayansi kwa vitendo iliyopo shuleni hapo, huku wakisimamiwa na Mwalimu John Mtafya ambaye alitoka nje kuendelea na shughuli nyingine za kimasomo.


Inaarifiwa kuwa Mwalimu huyo aliwaacha Wanafunzi hao wakiendelea na usafi na ndipo walipoingia katika chumba cha kuhifadhia Kemikali ambayo walichukua kemikali aina ya ethanol na kuinywa na baada ya kumaliza usafi waliendelea na masomo pasipo kusema chochote.

Wanafunzi wengine Evangelist Deodatus (20), mpaka sasa anaendelea na matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi na Anastasia Zakayo (17), hali yake ni njema na anaendelea na masomo.

TUPE MAONI YAKO HAPA
 
Support : Peruzibongo Admin Peruzibongo Kwa Habari MotoMoto Bila Kikomo
Copyright © 2009. Shikamoo Pesa - Haki Zote Zimehifadhiwa.
Sponsored by Mwanahabarihuru
Proudly powered by Blogger